Pages

Tuesday, November 17, 2015

LINGARD NA MASON WAITWA ENGLAND, VARDY NA CARRICK NJE DHIDI YA UFARANSA

England players
Wachezaji wa England wakisimama kimya kwa dakika moja kama ishara ya kuomboleza shambulizi lililotokea Paris wakati wa mazoezi ya timu hiyo jana kwenye Uwanja wa Einfiled.
Winga wa Manchester United Jesse Lingard ameitwa kwa mara ya kwanza kwenye kikosi cha wakubwa cha timu ya taifa ya England kitakachoivaa Ufaransa baada ya kuanza msimu huu wa Ligi ya Uingereza katika fomu nzuri. Pamoja naye yupo pia Ryan Mason wa Tottenham ambaye ametoka kupona majeraha yake muda si mrefu.
 Jesse Lingard and Ryan Mason playing for England Under-21s and England
Lingard, 22 amecheza mechi 11 za U21 lakini hakuwahi kuitwa kqwenye kikosi cha wakubwa. Mason alicheza mechi yake ya kikosi cha wakubwa mwaka huu mwezi March dhidi ya Italy.
Mshambuliaji aliye kwenye fomu ya juu kabisa Uingereza Jammie Vardy wa Leicester City ameachwa katika kikosi hicho kitakachovaana na France kwenye Uwanja wa Wembley hapo November 17.
Kiunghoi wa Manchester United Michael Carrick pia hatokuepo kwenye kikosi hicho kufuatia majeraha ya ekna aliyopata wiki iliyopita wakati England ikijipima nguvu dhidi ya Spain ingawa vipimo vimethibitisha kuwa jeraha lake sio la kumuweka nje ya uwan ja kwa muda mrefu.

No comments:

Post a Comment