Pages

Thursday, July 2, 2015

PROFILE YA EPIPHANIA TOWO..



Imeandaliwa na Jay4  
 Uchaguzi mkuu wa Raisi, wabunge na madiwani unakaribia ikiwa imebakia miezi kadhaa kufikia 25 Oktoba 2015. Wengi wamekuwa na maswali kichwani juu ya uandikishaji wa njia ya elektroniki (Biometric Voters Registration) kama itaweza kuandikisha Watanzania wote kwa muda uliopangwa. Mwanafunzi mahiri wa sheria anatoa majibu kuhusu mambo muhimu ya Uchaguzi mkuu na taaluma yake.

1.      Unaitwa nani?
Kwa majina yangu ya cheti nafahamika kama EPHANIA PIUS TOWO, nasomea kitivo cha Sheria mwaka wa pili. Natumia mitandao ya kijamii pia napatikana INSTAGRAM: FANIATOWO pia na FACEBOOK: EPIPHANIA  TOWO

Epiphania akiwa katika maandalizi ya mitihani ya mwisho.
2.      Uandikishwaji mpya  wa elektroniki kwa wapiga kura (BVR)  hususani kwa wanafunzi walioko Chuoni na muda wa Uchaguzi wanakuwa likizo ni haki?
“Hapana si HAKI, kwanza ni nafasi kubwa ya kunyimwa haki ya kuchagua na kuchaguliwa kama Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  inavyosema katika kifungu cha 21. Kwanza muda wa Uchaguzi wanafunzi wengi wanakuwa wako likizo majumbani kwao na wengi wanakuwa wametoka mikoa ya mbali tofauti na chuo wanaposomea. Muda ni mdogo kwa uandikishaji na hata kipindi cha uandikishaji wanafunzi tunakuwa katika kipindi cha masomo, serikali haileti usawa kwa kuwafikiria wanafunzi waliotoka ile mikoa iliopitiwa mfano Njombe, Lindi na Mtwara”. 

3.      Kwa taaluma yako ya sheria unaishauri nini Kamati ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)?
“Ushauri mkubwa ni kuwepo sheria yenye kutambua Kitambukisho maalumu  ambacho mwanafunzi atakipata kwa muda awapo chuoni na kumfanya apige kura mahala popote bila kuvunja sheria za upigaji kura mfano, kupiga kura mara mbili. Hii itasaidia kuendana na muda na kuwapa haki wanafunzi wa vyuo vikuu wote.”

4.      Kwanini kuna ufinyu wa namba  ya wanafunzi wa kike katika “Law school”?
“Hilo ni jambo kiukweli linaumiza, tunakuwa wengi sana katika ngazi ya shahada ila inapofikia ‘Law school’ namba kubwa inakuwa ni wanaume. Wengi huwa ni woga katika masomo ya ngazi hii kwa kupewa vitisho na waliotangulia katika ngazi hiyo japo sina uhakika sana. Ushauri kwa wanawake wote ni kupambana na kuhakikisha tunafika ‘Law school’ ili tuweke usawa katika jamii yetu hususani mawakili na wanaharakati amabapo wanaume wametawala sana”.

5.      Unavutiwa na mwanamke gani maarufu hapa Tanzania?
Dr. Asha-rose Migiro ni mwanamke natamani kuwa kama yeye au kuwa zaidi yake haswa katika sifa zote aliyoipa Tanzania na kutochoka katika uwajibikaje wa kazi za kila siku. Uhodari wake unanifanya kunivutia zaidi kufata nyayo zake”.

2 comments:

  1. Tupo vizuri sana lets keep this spirit up and up people, hurray

    ReplyDelete
  2. Asante sana mkuu, tutafikia malengo 1 day

    ReplyDelete