Pages

Monday, July 6, 2015

UKISTAAJABU YA MUSA UTAYAONA YA CHILE KOPA AMERIKA 2015.



Hakika kila lenye mwanzo halikosi kuwa na mwisho asilani,msemo huu umetimia siku ya jana baada ya wapenda soka wote duniani wakishuhudia kufungwa kwa pazia la  mashindano ya kopa Amerika yaliyokuwa yakitimua vumbi huku  nyasi za viwanja mbalimbali nchini Chile zikipatakukiona cha mtema kuni.

Mashindano hayo yalinogeshwa kwa ushiriki wa timu za Bolivia,Chile,Peru,Uruguay,Colombia,Paraguay,Brazili,Mexico,Jamaica na Argentina na nyingne nyingi yaliyaanza kwa kupooza lakini kadri siku zilivyokuwa zinasonga mbele ndivyo yalipopata kujizolea umaarufu kutokana na vituko kadha wa kadha sambamba  na ufundi wa hali ya juu ulikuwa unaonyeshwa na vijana kutoka bara hilo linalopatikana kusini mwa Amerika.




Kubwa zaidi ni kumuhusu kiungo wa timu ya taifa ya Chile na klabu ya Juventus ARTULO VIDAL kukamatwa kwa kusabisha ajali kutokana na unywaji wa pombe kupindukia siku chache kabla ya michuano hiyo kuanza,licha ya gari lake kuharibika vibaya lakini mwenyewe hakupatwa na majeraha yoyote.Tukio hili lilikuwa ni kama ndimu kwenye mchuzi kwani kwa upande wa pili liliwavutia wadau wa kandanda haswa wakitaka kufahamu wenyeji hao wengefanya yapi katika michuano hiyo.

Mshambuliaji wa timu ya Argentina Lionell Messi akishangalia bao.

Utamu wa mchuzi huo ulisabisha macho ya wapenda  soka kuelekezwa kwa nyota wa Barcelona na timu ya taifa ya Argentina si mwingine ni Yule mchezaji aliyezaliwa na kipaji kikubwa ch kusakata kabumbu LIONELL MESSI, licha ya kufikisha michezo 100  pamoja na kuchangia timu yake kuelekea  fainali,Kwa upande mwingine alishindwa kuisadia Argentina kutwaa ubingwa huo waliounyakua kwa  mara mwisho mnamo mwaka 1993.

Shombo liliingia katika mchuzi huo pale beki wa Chile na klabu ya mainz 04 GONZALO JARA kuwatibua wapenda soka kutoka na kitendo chake kisichokuwa cha kiungwana,mara baada ya kumchoma kidole mshambulia hatari wa Uruguay na PSG ya Ufaransa mkali EDINSON CAVANI.Kitendo hicho kilimpelekea beki wa Atletico Madrid DIEGO GODIN kulitaka shirikisho la soka barani humo kutoa adhabu kali kwa JARA, kama ilivyokuwa kwa LUIS SUAREZ pale alivyomngata beki wa Italia GEORGIO CHELLIN.Khali ilikaa sawa baada ya beki huyo kufungiwa kushiriki michezo iliyobakia ya timu yake.
Gonzalo Jara akionyesha utovu wa nidhamu kwa cavani.
Upekee wa mchuzi huo uliwashangaza wapenda soka na kuwaacha vinywa wazi pale waliposhuhudia Chile ikitwaaa kombe lake la kwanza katika historia ya soka ikiwa na wachezaji wenye viwango vya kisasa kama ALEXIS SANCHEZ anayekipiga na washika mitutu wa ARSENAL pamoja na kiungo mpambanaji ARTULO VIDAL ambaye unaweza kumfananisha na yule mkali wa sinema za kivita SILVESTER STALLON  wengi wanamuita RAMBO.

Chile walinyakua ndoo hiyo baada ya kuisukumiza nje ya mashindano hayo Argentina kwa mikwaju ya penalti  4 kwa 1 baada ya dakika 120 za mchezo huo kumalizika timu zote zikiwa suluhu ya kutokufungana.Argentina iliyokuwa chini  ya kocha TATA MARTINO watajilaumu kwa kukosa ubingwa huo licha ya kumiliki kikapu kilichokuwa na nyota wasioweza kuhesabika wakiwemo ANGEL DI MARIA,GONZALO HIGUAN,HAVIER PASTORE,LIONEL MESSI na SERGIO AGUERO.
Wachezaji wa timu ya Argentina wakijiaanda kupiga mikwaju ya penalti dhidi ya Chile.
Penalti za mabingwa hao ziliwekwa kambani na FERNANDEZ,VIDAL,SANCHEZ huku penalti ya kuondoa aibu kwa upande wa Argentina ilisukumizwa kambani na MESSI

Mabingwa wa kopa Amerika 2015 Chile wakishereheka kombe lao.
Mashindano hayo yalimaliza kwa Peru kuibuka kuwa timu yenye nidhamu kwenye michuano hiyo huku EDUARDO VARGAS tokea Chile na PAOLO GUERRERO kutoka Peru wakiondoka na kiatu cha dhahabu baada ya kuibuka wafungaji bora kwa kuwa na jumla ya magoli manne(4) kila mmoja.
Eduardo Vargas wa Chile akisherekea moja ya goli alilotupia.
Hakika kwa wale mashabiki walevi wa mashindano haya tukutane tena mwakani kule nchini marekani.Ila utakubaliana nami kuwa mashindano ya mwaka huu yalikuwa na utamu wa aina yake au sio???.TUKUTANE PALEE VIGOGONI KWA MASTORI MENGI MENGI.

Nembo itakayotumika katika mashindano hayo mwakani nchini Marekani.



No comments:

Post a Comment