Pages

Friday, June 26, 2015

PROFILE YA JACKSON SHEKI..



Imeandikwa na Jay4.  

 Wahenga walisema,” kwenye wengi pana mengi”. Ndio hali nimekutana nayo katika wanafunzi wengi wa Chuo cha Tumaini Dar es Salaam. Katika uwingi wao nikakutana na  kijana shupavu, mcheshi kwa kila mmoja, aliebarikiwa fikra za mabadiliko kuhusiana na Chuo cha Tumaini Dar es Salaam. Alijibu maswali matano kiufasaha nilipomuuliza katika mahojiano.
1.      Unaitwa nani?
Kwa majina nafahamika kama JACKSON SIMON SHEKIGENDA, nipo mwaka wa pili kitivo cha Rasilimali watu (HUMAN RESOURCE MANAGEMENT). Napatikana katika mitandao ya kijamii kama FACEBOOK kama SHEKI_JR na INSTAGRAM kama SHECK DIASPORA.  

2.      Ni kitu gani umekiona muhimu katika vyuo vikuu vingine na ungependa kiwe miongoni mwa huduma katika Chuo cha Tumaini?
Akiwa katika maandalizi ya mitihani ya mwisho.( Picha na Jay4)
Kwa kutumia mfano wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam, kuna mambo mawili muhimu, la kwanza ni uwepo wa semina ambazo hufanyika baada ya muda wa masomo darasani, zinaruhusu wanafunzi kuuliza maswali na kueleza kiasi gani waeelewa. La pili ni kutokuwepo kwa hosteli, wanafunzi tunapata tabu kwenda kupanga vyumba kwa bei ya juu tofauti na Chuo kikuu cha Dar es Salaam ambao wana hosteli nzuri na zilizo ndani ya Chuo, ningependa sana na hapa zijengwe hata kama si mimi niwe mtumiaji bali hata kwa vizazi vinavyokuja katika Chuo hiki kizuri.
 
3.      Kulalamikiwa kwa sekta ya burudani Chuoni, unaishauri kipi serikali ya wanafunzi (TUSODARCO)?
Kwanza tumekosa ushirikiano na vyuo vingine ambavyo huwa na utaratibu wa kuungana na kuandaa burudani itakayotuleta pamoja, kwahiyo uongozi lazima uweke ushirikiano na vyuo amabavyo vinaleta wanafunzi pamoja katika burudani. Pia, wanafunzi tumetofautiana katika hulka ya kupenda huduma tofauti katika burudani, kwa mfano mimi ni mpenzi wa muziki ningeshauri kila baada ya mitihani watuwekee burudani ya muziki ‘kujipoza’ na mitihani.
4.      Katika huduma nyingi zinazotolewa na Chuo Cha Tumaini, Je huduma gani umeifurahia sana?
Nisiwe mnafiki, uongo dhambi. Huduma ipo kubwa na sijui kama sehemu nyingine ipo, ni jinsi walimu wanavyotujali katika ufundishaji wanakuwa kama marafiki, wanatupa taarifa na uzoefu  kadri ya uwezo wao ili kutufanya kuwa wanafunzi bora zaidi. Ukaribu huu unanifanya nijisikie amani zaidi katika masomo yangu.
5.      Mwalimu gani katika kozi yako unamuelewa sana?
Walimu wote nawaelewa ila zaidi namuelewa Dr. Ngirwa, kwakuwa ni zaidi ya mwalimu namchukulia kama babu yangu.  Vilevile nje ya darasa pia, hata uwe na tatizo unaweza kumfata na akakupa ushauri mzuri sana. Kiukweli nampenda sana.

3 comments: