Pages

Tuesday, July 7, 2015

MASIKINIII!!!! MYWEATHER, YAMEMFIKAAA HAPAA.



Bondia maarufu kutoka nchini Marekani ambaye anaeshikilia rekodi ya kucheza michezo mingi ya masumbwi bila kudundwa brazameni na bishoo FLOYD MONEY MYWEATHER 38,amenyanganywa ubingwa welterweight pamoja na kutokutambulika kama bingwa katika shirikisho la ngumi duniani(WBO).
Myweather pichani akiwa na mataji yake matatu.
Tukio hilo limetokana na MYWEATHER kuvunja sheria  zinazoungoza mchezo huo wa masumbwi zilizomtaka,mosi kulipa ada ya ushiriki wa ubingwa huo  kiasi cha $200,000 katika siku ya ijumaa iliyopita kutokana  pambano lake la mei 2 dhidi ya Mfilipino MANNY PACQUIAO .Pili kukiuka kanuni inayokataa bingwa wa shiriksho hilo kupambana na kushikilia mikanda ya  uzani zaidi ya mmoja.

Myweather akimbonyeza mwenzie kizenji.
Kabla ya kupokonywa ubingwa huo wa (WBO) MYWEATHER alikuwa anashikilia mikanda ya uzani tofauti ikiwemo welterweight kutoka WBC pamoja  na ule wa super welterweight kutoka shirikisho la WBA


Licha kupewa adhabu hiyo kamati ya shirikisho hilo imempatia kibali cha siku 14 bondia huyo kukata rufaa kutokana na maamuzi yaliyochukuliwa,kama kanuni ya za mchezo huo inavyoelekeza katika ibara ya 34 ibara ndogo ya 3(e) ikiwa bondia hajaridhishwa na maamuzi ya shirikisho hilo ataruhusiwa kukata rufaa kwa kipindi kisichozidi siku 14 na kuiwasilisha kwa rais wa shirikisho hilo.

watoto wa mujini  wanakwambia ni checheeeee.Myweather akikiona cha moto kutoka kwa Pacquiao.
IKUMBUKWE ushindi wa mataji hayo matatu kwa bondia huyo yalipatikana kimagumashi  tarehe 2 ya mwezi mei dhidi ya PACQUIAO ulikuwa ukilalamikiwa na wapenda masumbwi kote duniani ,Hivyo majanga hayo yametafsiriwa kama ni matokeo ya laana kutoka kwa PAC MAN.

             IMELETWA KWENU: KWA HISANI YA WATU KUTOKA KIBENCHI MAWAZO…011.

No comments:

Post a Comment