Pages

Thursday, June 18, 2015

VIROBA VYA ZIBA VYOO



Wanafunzi wa chuo Kikuu  Tumaini cha jijini Dar es salaam wameulalamikia uongozi wa chuo hicho kutokana miundombinu mibovu ya vyoo chuoni hapa hasa katika jengo jipya.

Wakiongea na mwandishi wa blogi hii, mmoja wa wanafunzi Jumanne Muyonga anaesomea SHAHADA YA MAWASILIANO mwaka wa pili amesema  “nimepata shida sana kwani kila ghorofa ninayoenda imefungwa na ilinibidi niende nje kwenye maliwato ya zamani kupata huduma..

Kwa upande wa mratibu wa jengo hilo Bwana Godfrey, amesema tatizo la kuziba kwa mabomba ya maji machafu ambayo lilitokana na mifuko ya pombe maarufu kama viroba. na wametatua tatizo hilo na hakuna shida tena wanafunzi wanaweza kuendelea kutumia kama kawaida.

Bwana Godfrey ametoa wito kwa  wanafunzi na watumiaji wahuduma za maliwato kuwa makini na kutunza miundombinu iliyopo kwani ikiharibika inatumika gharama kubwa kuikarabati.

Mfano wa viroba vilivyo sababisha vyoo kuziba.
Moja ya choo katika jengo jipya.










No comments:

Post a Comment