Pages

Thursday, June 18, 2015

WALINZI WAOMBA USHIRIKIANO




Walinzi wa chuo Kikuu Tumaini cha Jijini Dar es salaam wametoa wito kwa uongozi wa chuo kuwa na ushirikiano katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Akiongea na mwandishi wa Blogi hii, mmoja ya walinzi alisema “tumepewa majukumu mengi sana ambapo ni pamoja na kuwakagua wanafunzi endapo wanavitambulisho halali vya chuo au la, lengo ni kugundua yupi mwanafunzi na yupi si mwanafunzi. Lakini baadhi ya wanafunzi wanakataa kukaguliwa na tukiwapeleka kwa Afisa Rasilimali Watu Bw Mwita hawachukuliwi hatua yeyote”.

Kwa upande wake afisa rasilimali watu Bw Mwita amesema walinzi hawawatendei haki wanafunzi kwani kitendo cha kusahau kitambulisho ni kawaida kwa binadamu, hivyo si utu kumzuia mwanafunzi kuingia ndani kwani wengine wanakua katika kipindi cha mitihani.

Hata hivyo wanafunzi nao wanawalaumu walinzi kwa kutokua makini na kazi yao. Wengine wanasema wanafunzi hawafuati sheria za chuo na wanawatendea vibaya walinzi na kuwadharau kutokana na kazi wanayofanya.


 
 Mlinzi akiwa kazini






No comments:

Post a Comment