Pages

Friday, September 18, 2015

SHAW NJE MIEZI SITA,VAN GAAL AINUNIA UEFA HUKU RONALDO AKIVUNJA REKODI ZAIDI.

Carragher on Shaw injury
Beki namba tatu wa Manchester United, Luke Shaw atakua nje ya uwanja kwa muda wa miezi hadi sita baada ya kuvunjika mguu kufuatia rafu mbaya aliyochezewa na beki wa PSV Eindhoven katika mechi ya awali ya Ligi Mabingwa Ulaya siku nne zilizopita.
Shaw alichezewa rafu mbaya na Hector Moreno katika eneo la hatari wakati beki huyo akijaribu kufunga katika mechi ambayo United ililala kwa mabao 2-1.
Shaw alitibiwa kwa dakika 10 uwanjani huku akiwa amewekewa kifaa cha kupumulia cha oksijeni kabla ya kukimbizwa hospitali ambapo alitibiwa haraka ili kupunguza maumivu kabla hajasafirishwa kurejea Manchester kwa matibabu zaidi.
Mwamuzi wa mchezo huo hakumuadhibu Moreno jambo lililomkera kocha Luis van Gaal na kitendo cha UEFA kumtangaza Moreno kama mchezaji bora wa mechi ndiyo kimeongeza hasira kwa kocha huyo Mdachi.
Memphis Depay aliifunga timu yake ya zamani dakika ya kabla ya Moreno kupiga kichwa kilichomgonga Daley Blind na kuzama wavuni kabla ya mapumziko.
Narsingh aliifungia PSV bao la ushindi katika kipindi cha pili na kuongeza maumivu kwenye benchi la United baada ya mkasa wa Shaw.
Nchini Hispania Real Madrid iliialika Shaktar Donetsk katika dimba la Santiago Bernabeu kabla ya Ronaldo kuibuka shujaa akifunga magoli matatu na Benzema akimalizia moja kufanya jumla ifike 4-0.
Kwa magoli hayo Ronaldo amemzidi mpinzani wake wa karibu Leonel Messi katika wafungaji wa Ulaya kwa kufikisha goli 80 huku Messi akibakia hatua tatu nyuma.
Mechi hiyo ilishuhudia Sergio Ramos, Gareth Bale na Rafael Varane wakipata majeraha yaliyolazimu kutolewa nje. Rafael Benitez amesema hawajajua rasmi jeraha la Bale litapona huku Ramos akiugulia maumivu ya bega.

Leonel Messi alishindwa kufunga wakati timu yake ikimenyana na AS R oma pale Stadio Olympico katika mechi yake ya100 kwenye michuano hiyo.
Messi anavunja rekodi ya kufikisha mechi hizo kama mchezaji mdogo zaidi kwenye orodha ya wachezaji 33 waliovuka mechi 100 za UEFA.
Luis Suarez alifunga bao la kuongoza kabla ya Florenzi kufunga goli la jabu la umbali wa mita 51.
Matokeo ya mechi zingine ilikua kama ifuatavyo;
UEFA Champions League
Jumatano, September 16, 2015
FT
TSV Bayer 04 LeverkusenBayer Leverkusen
4 - 1
FC BATE BorisovBATE
FT
Chelsea FCChelsea
4 - 0
Maccabi Tel Aviv FCMaccabi Tel Aviv
FT
GNK Dinamo ZagrebDinamo Zagreb
2 - 1
Arsenal FCArsenal
FT
FC Dynamo KyivDynamo Kyiv
2 - 2
FC PortoPorto
FT
KAA GentGent
1 - 1
Olympique LyonnaisOlympique Lyonnais
FT
Olympiakos CFPOlympiakos Piraeus
0 - 3
FC Bayern MünchenBayern München
FT
AS RomaRoma
1 - 1
FC BarcelonaBarcelona
FT
Valencia Club de FútbolValencia
2 - 3
FK Zenit St. PetersburgZenit
Jumanne, September 15, 2015
FT
SL BenficaBenfica
2 - 0
FK AstanaAstana
FT
Galatasaray SKGalatasaray
0 - 2
Club Atlético de MadridAtlético Madrid
FT
Manchester City FCManchester City
1 - 2
Juventus FCJuventus
FT
Paris Saint-Germain FCPSG
2 - 0
Malmö FFMalmö FF
FT
PSV EindhovenPSV
2 - 1
Manchester United FCManchester United
FT
Real Madrid Club de FútbolReal Madrid
4 - 0
FC Shakhtar DonetskShakhtar Donetsk
FT
Sevilla FCSevilla
3 - 0
Borussia VfL MönchengladbachBorussia M'gladbach
FT
VfL WolfsburgWolfsburg
1 - 0
PFK CSKA MoskvaCSKA Moskva





No comments:

Post a Comment