Pages

Friday, August 7, 2015

WASIFU WA MGOMBEA URAIS WA ADC


Chifu Yemba ni nani?
Chifu Yemba ambaye ni mwenyeji wa mkoa wa Kigoma, alizaliwa Mbinga mkoani Ruvuma mwaka 1966. Alisoma shule ya msingi ya Kaluta kati ya mwaka 1975 na 1981. 

Alisoma shule za sekondari za Uyui na Ujiji kati ya mwaka 1982 na 1985. Mwaka 1986 hadi 1987 alisoma kidato cha tano na cha sita katika shule ya Sekondari ya Iyunga mkoani Mbeya.
Kati ya mwaka 1988 hadi 1990 alisoma katika Chuo Kikuu cha Southern Carolina na kutunukiwa shahada ya elimu ya viumbe.

Mwaka 1998 alisoma katika Chuo Kikuu cha Frankfurt, Ujerumani na kupata Shahada ya Uzamili ya Hydrogas. Kisiasa aliwahi kuwa mwanachama wa CUF kabla hajahamia katika ADC.

Aliwahi kufanya kazi katika halmashauri ya Kigoma, Ujiji kati ya mwaka 1987 hadi 1997.Hivi sasa ni mjasiriamali anayejishughulisha na uchimbaji wa madini.

No comments:

Post a Comment