Pages

Monday, August 3, 2015

NGUVU YA EDWARD LOWASSA NDANI YA UKAWA



Edward Lowassa mgombea uraisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chadema

Mgombea uraisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), pamoja na muunganiko wa vyama vinavyounda  umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA), Edward Ngoyai Lowassa amesafishwa na wanasheria pamoja na wachambuzi mbalimbali wa siasa hapa nchini.

Wakihojiwa na kituo kimoja cha habari cha Ujerumani cha radio DOTCH VERE,  kuhusu mstakabali wa Edward Lowassa kujiunga na UKAWA. kila mmoja alionesha kuwa Edward Lowassa yuko upande sahihi na hajakosea kwa kuzingatia kauli mbiu yake ya “safari ya matumaini”, na   kwamba haiwezi kupatikana ndani ya chama cha Mapinduzi ila kupitia ukawa. Ifahamike kuwa Edward Lowassa amejiunga na chadema na kukubaliwa kuchukua fomu ya kuwania nafasi ndani ya ukawa ili aweze kuchaguliwa na wananchi kuwa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, baada ya jina lake kukatwa katika mchujo uliofanyika huko Dodoma kwa chama chake cha awali cha Mapinduzi. (CCM).

Mdau wa kwanza ni Tundu lisu, mbunge wa jimbo la Singida Mashariki na ni mwanasheria mkuu wa chadema, amemzungumzia Edward Lowassa Katika sakata la RICHMOND kuwa alishiriki kama waziri mkuu na alichukua uamuzi wa kujiuzulu kutokana na nafasi aliyokuwa nayo wakati huo, Na yeye kwa
kutambua hilo aliamua kuwajibika kisiasa kwa kuchukua uamuzi wa kujiuzuru wadhifa wake.

Tundu Lissu Mwanasheria mkuu wa CHADEMA(Katikati)
Ameongeza kuwa bunge “liliunda tume ya kuchunguza sakata hilo lakini ikaja kufahamika kwamba Edward Lowassa alikuwa hausiki na kashfa hiyo, na kama alikuwa anahusika kwa nini serikali haikumchukulia hatua ya kumshtaki?”  Alihoji Tundu Lisu.

Hata hivyo ameongeza kuwa, ndani ya chadema hakuna na hakutakuwa na mpasuko wowote kwani Edward Lowassa hajaokotwa tu jana au juzi ni muda mrefu wa miezi mitatu iliyopita mpaka wakafikia muafaka kuwa akubaliwe katika chama. Makubaliano hayo yalifanywa na viongozi wote wa chama wakuu ambao ni Mwenyekiti, katibu mkuu wa chama,  na viongozi wengine wa chama. 

Mdau mwingine aliyechangia ni Yusuf Kamoti ambaye ni mchambuzi wa siasa amesema, “uchaguzi wowote, katika nchi yoyote, katika jamii ya watu wowote unapotokea ni jambo la jaribio kwa wanadamu wanaoishi katika eneo husika” amesema hivyo kwa sababu mgombea ambae anatarajiwa kupitishwa na Ukawa ni Edward Lowassa na hili ni jaribio kwa wananchi wa Tanzania.

Mwakilishi wa jimbo la Mji Mkongwe (CUF) Ismail Jusa
Mdau  mwingine aliyechangia, ni mwakilishi wa baraza la wawakilishi na ni mbunge wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka katika jimbo la Mji Mkongwe, Ismaili Jussa, amesema kuwa, mojawapo ya sifa ya siasa ni “dynamic” katika maana  ya kwamba siasa inabadilika kadiri ya nyakati na mahitaji. Kwa kitendo cha Edward Lowassa kujiunga na chama cha upinzani ni jambo la kawaida, na si Tanzania tu bali ni duniani kote.

Alipotangaza nia ya kugombania kiti cha uraisi jijini Arusha kupitia chama cha Mapinduzi alizitaja agenda ambazo zinafanana kabisa na agenda za ukawa ambazo ni kufufua uchumi, kupambana na ufisadi pamoja na rushwa, kuongeza ajira kwa vijana na kutumia rasilimali za nchi kwa manufaa ya wananchi wote wa Tanzania, hizo ni baadhi tu ya agenda za Lowassa na ndizo zinazofanana na Agenda za UKAWA, pia katika suala la katiba mpya atazingatia maoni ya Wananchi na sio maoni ya watu wachache, hivyo ndivyo Ismaail Jussa alivyomzungumzia Edward Lowassa.

wafuasi wa Edward Lowassa, kauli mbiu yao ni "popote tupo"
Mdau wa mwisho kuchangia mada ni Aguta Mussa, ni mchambuzi wa siasa nchini Tanzania, kwa upande wake alisema, kitendo cha Edwarrd Lowassa kujiunga na upinzani ni tofauti na kitendo alichokifanya Augustino Lyatonga  Mrema ambaye alihama Chama cha Mapinduzi na kujiunga na chama cha NCCR-Mageuzi akitegemea kupata kiti cha uraisi kupitia upinzani, lakini haikuwezekana. Utofauti mkubwa uliopo kati ya hawa wawili ni kwamba Edward Lowassa kajiunga na ukawa wakati tayari ukawa walikuwa wamekwishakubaliana kujiunga pamoja na kumpata mgombea mmoja wa uraisi, hivyo kuja kwa Edward Lowassa kunaongeza nguvu kubwa ya wananchi ambao walikuwa wanapenda Lowassa kuwa raisi kupitia CCM, na kwa bahati mbaya hakupitishwa. Hivyo watu walewale wa CCM wako na watakuwa tayari kumchagua Edward Lowassa kuwa raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hata kama yuko upande wa UKAWA.

Mwisho wa siku ni hapo Oktoba 25 mwaka huu ambapo wananchi watachukua uamuzi wa kumchagua raisi mmojawapo kati ya Edward Lowassa, John Magufuli na wagombea wengine kutoka katika vyama vingine vya upinzani.








No comments:

Post a Comment