Pages

Saturday, August 1, 2015

RAISI MPYA WA TANZANIA NI KATI YA HAWA WAWILI



Wakati mbio za uchaguzi mkuu wa uraisi, ubunge na udiwani zikipamba  moto katika kila kona ya nchi, wagombea na wafuasi wao wakijigamba kushinda kwa kishindo katika uchaguzi mkuu utakaofanyika hapo Oktoba 25,2015.
 
mgombea uraisi kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Edward Ngoyai Lowassa akiwa na mkewe Bi. Regina Lowassa mara tu walipokabidhiwa kadi za chama
John Pombe Magufuli ni mgombea wa uraisi kupitia  Chama cha Mapinduzi (CCM)  anatarajia kupata upinzani mkubwa kutoka katika vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA)  ambavyo ni CHADEMA, CUF, NCCR-MAGEUZI na NLD.

          Dr. John Pombe Magufuli   mgombea kiti cha uraisi kupitia chama cha Mapinduzi














Kwa upande wa chama cha Mapinduzi kesho tarehe 01/08/2015 ndiyo siku ya kuchaguliwa wabunge wao waliotangaza nia ya kugombea ubunge kwa majimbo husika. Kwa lugha nyingine tunaweza kusema kwamba, kesho ni siku pekee ya kukatwa kwa baadhi ya waliotangaza  nia na wachache wao kupitishwa.


mgombea uraisi kupitia chama cha demokrasia na maendeleo, Edward Ngoyai Lowassa akisisitiza jambo kuwa ana imani na ukawa pia ana imani na ushindi hapo Oktoba 25 mwaka huu.

Kwa upande wa ukawa wamekwisha gawana majimbo mbalimbali kwa kuzingatia chama gani kinakubalika mahali gani.  Lowassa pamoja na Ibrahim Lipumba ni wagombea pekee kwa upande wa ukawa,  mmoja wao atapata nafasi ya kupeperusha bendera ya umoja huo.
 


Hawa ni baadhi ya watu wanaojiita team Lowassa popote aendapo nao wapo, anaonekana msichana shupavu Christina Mshiu ambae ni msomi wa chuo kikuu.

Ni nani atakayekuwa raisi kati ya hao wawili  ni kutokana na maamuzi ya wananchi hapo Oktoba 25 mwaka huu, endapo Edward Lowassa atashinda kiti cha uraisi atakua ni kiongozi wa kwanza kutoka chama cha upinzani kushika dola na atakuwa ni waziri mkuu wa pili kuwa raisi, wakati waziri mkuu wa kwanza ni Hayati Mwalimu J.K. Nyerere na baadaye akawa raisi wa kwanza wa Tanzania akitokea katika wadhifa wa uwadhiri mkuu, kwani baada ya yeye mawaziri wakuu wote walioomba ridhaa kupitia chama chao cha Mapinduzi walikatwa..

No comments:

Post a Comment