Pages

Friday, August 28, 2015

MANCHESTER KICHEKO, REAL MADRID PAGUMU UEFA CHAMPIONS LEAGUE




UEFA Champuions League inarudi tena, Jana imefanyika droo ya kuoanga makundi baada ya kumaklizika kwa mechi za mchujo jumanne na jumatano iliopita ambapo tulishuhudia kurudi kwa Manchester United iliyoifunga Club Brugge ya Belgium.


Real Madrid watapata wakati mgumu kama anavyosema staa wao Cristiano Ronaldo baada ya kupangwa group moja na Paris Saint Germain, Shaktar Donetski na Malmo FC. PSG wametumia pesa nyingi kwa misimu ya karibuni lengo lao kuu ikiwa ni kuuchukua ubingwa wa Ulaya.
Group hili litashuhudia nguli wa soka Zlatan Ibrahimovich akirudi katika klabu yake ya zamani, Malmo.


Manchester United wanaonekana kuppata group laini baada ya kutupwa kwa PSV ya Uholanzi, Wolfsburg na CSKA Moscow. Winga mpya wa Manchester United Memphis Depay atarudi katika uwanja uliomlea safari hii akiwa na jezi za mashetani wekundu na sio PSV tena.

Majirani zao Arsenal wana kibarua kigumu baada ya kuwekwa kundi moja na Bayern Munich ambayo wamekutana mfululizo kwenye miaka ya karibuni. Makundoi yote ni kama ifuatavyo.

  • Group A: Paris St-Germain, Real Madrid, Shakhtar Donetsk, Malmo
  • Group B: PSV Eindhoven, Manchester United, CSKA Moscow, VfL Wolfsburg
  • Group C: Benfica, Atletico Madrid, Galatasaray, Astana
  • Group D: Juventus, Manchester City, Sevilla, Borussia Monchengladbach
  • Group E: Barcelona, Bayer Leverkusen, AS Roma, BATE Borisov
  • Group F: Bayern Munich, Arsenal, Olympiakos, Dinamo Zagreb
  • Group G: Chelsea, Porto, Dynamo Kiev, Maccabi Tel-Aviv
  • Group H: Zenit St Petersburg, Valencia, Olympique Lyon, Gent

No comments:

Post a Comment