Pages

Wednesday, June 24, 2015

PROFILE YA EVELYN



  
Katika pozi la picha baada ya mahojiano na mwandishi.

 Karibu sana katika kipengele maalumu kilichoandaliwa na Mwanafunzi Muyonga Jumanne (JAY 4). Dhumuni ya hiki kipengele ni kupata taarifa katika maswali matano (5) kuhusiana na mada tofauti kama taaluma, burudani na jamii inayomzunguka katika Chuo Kikuu cha Tumaini Dar Es Salaam.

     1. UNAITWA NANI?
 "Naitwa EVELYN GASPER, nipo mwaka wa pili kitivo cha mawasiliano kwa umma (mass communication). Napatikana Instagram GEVELIYM          au               Facebook         -
EVE GASPER".

  2.UNAIZUNGUMZIAJE TUDARCO?
"Ni moja ya Chuo kizuri katika vyuo bora Tanzania, kimenipa kujua mengi ambayo sikuweza jua kipindi cha nyuma. Nimejua mengi katika masomo na mazingirayanayonizunguka hapa Chuoni".

 3.USHAURI JUU YA TUDARCO?
"Nina mambo mawili ya kushauri katika kuboresha Chuo changu cha Tumaini, la kwanza ni upatikanaji wa namba za mtihani, naweza sema zinashusha ufaulu wa wanafunzi kwakuwa wengi wanakosa muda wa kujiandaa vizuri kimawazo kwa kuwaza jinsi ya kupata namba. Chuo kiweke utaratibu mzuri wa upatikanaji namba kwa mtu alielipa mapema. La pili ni ufinyu wa upatikanaji wa vitabu vya kukidhi mahitaji ya wanafunzi katika maktaba, ningeshauri Chuo kipate vitabu vya kutosha".

4.  UNAJIVUNIA AU HUJIVUNII KUWA MWANAFUNZI WA TUMAINI? KWANINI?
"Ndio najivunia, kwanza najivunia kwa kupata nafasi ya kuchaguliwa hapa si wote waliotamani kusoma hapa wamepata nafasi hiyo. Pili ni maarifa ambayo nimeyapata hapa Chuoni yameweza kunisaidia mpaka sasa naweza kusimama mtaani na kuonekana msomi huku uwezo wa kufanya jambo kama msomi umeongezeka pia zaidi. Nitajivunia miaka yote kuwa mmoja wa wanafunzi wa Tumaini, Dar es Salaam".
 
5. KWANINI MAWASILIANO KWA UMMA (MASS COMMUNICATION) NA SIO KOZI NYINGINE?
 "Nimechagua kusoma Mawasiliano kwa Umma kwanza ni kozi yenye wigo mkubwa katika usomaji, tofauti na watu wanavyozani kuwa ni uhandishi wa habari. Pia nitakuwa mwakilishi wa sauti kwa wale wasiosikika na wale wenye kuonewa".

1 comment: