Pages

Thursday, June 25, 2015

KUELEKEA UE, FAHAMU ZAIDI KUTOKA UHASIBU (NEW! NEW! NEW!) MPYA



Mhasibu wa Tudarco, Yvonne Mmbando akisisitiza jambo ofisini kwake.

Wanafunzi wametakiwa kulipa ada mapema ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza kuelekea maandalizi ya mitihani yao.

Hayo yamezungumzwa na  Mhasibu wa Chuo cha Tumaini Dar es salaam YVONNE MMBANDO, wakati akitolea maelezo kuhusu upatikanaji wa namba za mtihani ambazo zitaanza kutolewa kuanzia Jumatatu ya  Juni 26 mwaka huu, huku mitihani ikitarajiwa kuanza July 6 mwaka huu.

Ada ya mwaka wa kwanza ni Tshs 2,405,000, mwaka wa pili Tshs 2,330,000 na mwaka wa tatu Tshs 2,365,000. Pamoja na ada wanafunzi wote wanatakiwa wawe wamelipa hela ya TCU Tshs 20,000 na TUSO Tshs 25,000.

Ameongeza kuwa kwa wale ambao wanaona hawataweza kulipa ada kwa wakati ni vizuri wakaandika barua kwenda kwa DPAA, majuma mawili kabla, ili kupata kibali cha kufanya mtihani maalum (special exams). akaunti za benki ambazo wanafunzi wanaweza kuzitumia kulipa ada ni pamoja na Akaunti ya CRDB 01J1021002200 na ya NBC ni 011103030931 hizini kwa ada ya chuo na TCU huku akaunti ya TUSO ikiwa ni CRDB 0150021957100

No comments:

Post a Comment