Pages

Friday, June 26, 2015

GAZEBO LA TIGO KUTINGA CHUO IJUMAA 26 JUNI 2015


Nasibu Mahinya balozi wa Tigo
Kumekuwa  na jumbe fupi zikitumwa na mtandao wa Tigo kwa wanafunzi kuhusu kujiandikisha kwenye gazebo ambapo jumbe hizo zinaelekeza kuwa kwa kujiandikisha kwenye Gazebo hilo kutapelekea kuendele kufurahia vifurushi vya chuo  kwa wanachuo watakapo kuwa likizo.

Ujumbe huo mfupi umekuwa ukitafasiriwa vibaya na baadhi ya wanafunzi na kufikiri kuwa kifurushi hicho kitapelekea wao kutojiunga tena na vifurushi vya tigo spesheli kwa wanafunzi kama University offers.

Akizungumza na mwandishi wa Blog hii Balozi wa Tigo Nasibu Mahinya amesema kuwa taarifa zinazo zushwa kuwa kwa kujiandikisha kwenye Gazebo la tigo kutazuia kujiunga na vifurushi vya chuo kikuu ni uongo kwani kwa kujiandikisha kwenye Gazebo la Tigo utapata nafasi ya kumpigia rafiki yako alie mbali na chuo kipindi cha likizo kwa gharama ya 2000 kwa mwezi lakini sio kujitoa kwenye vifurushi vya University offer.

Kuhusu Gazebo kuja Chuoni Nasibu amesema huenda kuanzia kesho tarehe 26 juni 2015 zoezi linaweza kuanza chuoni muhimu ni kufika na kitambulisho chako na utaandikishwa moja kwa moja kwenye Gazebo hilo.

No comments:

Post a Comment