Pages

Monday, June 22, 2015

MAUA YAMEKUA DILI MJINI



Kutokana na kukithiri kwa tatizo la ajira nchini, vijana wengi wameamua kujishughulisha na shughuli mbalimbali za uzalishaji mali ili kujipatia kipato na kuondokana na njia haramu ya kujipatia mali.

Mmoja wa wajasiriamali ambae anajulikana kwa jina la Bariki Blastus anayejishughulisha na upandaji  wa aina mbalimbali za maua katika eneo la pembeni ya Chuo Kikuu cha Tumaini,  amelezea faida kubwa anayoipata katika shughuli yake ya upandaji na uuzaji wa maua.

Ameongeza kuwa, kutokanana kazi anayoifanya anaingiza kiasi kikubwa cha fedha kwani kwa siku anaweza kuuza miche ishirini hadi hamsini, na kila mche una bei yake kuanzia shilingi elfu mbili hadi elfu kumi.

Ameeleza kuwa,  kutokana na kazi anayoifanya anaweza kujikimu na mahitaji yake yote ya msingi kama vile chakula, malazi na mavazi na hata kutoa msaada kwa ndugu zake pindi wanapokua na shida mbalimbali za kifedha.

Kutokana na faida kubwa anayoipata, amebainisha changamoto kadhaa ambazo anakumbana nazo katika majukumu yake ya kila siku ambayo ni pamoja na kutokuwepo kwa maji ya uhakika kwani mara nyingi yanakuwa ni ya msimu, kukosekana kwa wateja  kwani mpaka maua yanakua makubwa na yanakomaa na kutofaa tena kwa kuuza, na pia hali ya hewa pia ni changamoto, kwani sio maua yote ambayo yanahimili hali ya hewa ya joto.

Hata hivyo, amewaasa vijana wengine kujitafutia shughuli za kufanya ili kuweza kujipatia kipato chao halali na kuondokan na njia haramu za upataji wa fedha kama vile uporaji na unyang’anyi.



mkulima wa maua akipalili bustani yake

No comments:

Post a Comment