Pages

Friday, June 26, 2015

KUTANA NA BEKI KATILI DUNIANI GONZALO JARA.



Gonzalo Jara akionyesha utovu wa nidhamu dhidi ya mchezaji mwezie Edinson Cavani
Wakati duniani ikishangazwa na kitendo cha ajabu na kisichokuwa cha kiungwana michezoni kilichotokea usiku wa jana katika mchezo wa robo fainali ya mashindano ya kopa Amerika, kwa beki wa timu ya Taifa ya Chile GONZALO JARA kumchoma kidole mshambuliaji wa  Uruguay na Paris saint German(PSG) EDINSON CAVAN,Wadau wengi wengi wa soka kote duniani wamekuwa na maoni mbalimbali kuhusiana na tukio hilo. Licha ya adhabu kali iliyotolewa na shirikisho la soka barani humo kwa kumfungia mechi zote zilizosalia za mashindano hayo. 

Kwa majina yake halisi anafahamika kama Gonzalo Alejandro Jara Reyes,alizaliwa mnano mwaka 1985 tarehe 29 ya mwezi agosti katika mji wa Santiago nchini Chile,alifanikiwa kuanza kuichezea timu ya taifa tokea mwaka 2006.Mpaka hivi sasa anacheza soka la kulipwa nchini Ufaransa katika klabu ya Mainz 05.

Luis Suarez (9) akimtwanga ngumi Gonzalez Jara(18)
Kunako mwaka 2004 katika mashindano hayo mshambuliaji mwingine  mtukutu toka Uruguay LUIS SUAREZ alishutumiwa kwa kumpiga ngumi JARA,tukio lililokuja baada ya mlinzi huyo kuanza kurushiana maneno na baadae kutaka kujaribu kumshika nyota huyo wa zamani wa klabu ya Liverpool wakati akiwa katika purukushani za kutafuta bao.Pia anakumbukwa zaidi na mashabiki wa Chile kwa penalti yake kugonga mwamba, katika mchezo wa robo fainali ya mashindano ya kopa Amerika mwaka huohuo na kuipatia nafasi Brazil kufudhu katika hatua ya Nusu fainaili ya mashindano hayo.

Penalti iliyopigwa na Jara ikigonga besela na kuitupa nje ya mashindano timu yake ya Uruguay

Taarifa kutoka katika mtandao mmoja wa nchini Hispania unaofahamika kwa  jina la Latercera,zinadai tofauti na wachezaji wengine wenye idadi kubwa ya wapenzi,Mlinzi huyo akiwa na umri wa miaka 19 aliweza kumuoa mpenzi wake ROXANA,na kufanikiwa kupata watoto wawili wa  kiume NICOLAS pamoja na LUCAS.

Jara akiwa na mkewe Roxana.
 Ikumbukwe mpaka  GONZALO JARA anakumbwa na kashfa hii,amekwisha kuzichezea timu mbalimbali za kulipwa barani Ulaya zikiwemo West Bromwich Albino(2009-2013) pamoja na Northingham Forest(2013-14) za nchini Uingereza.



No comments:

Post a Comment