Pages

Friday, November 27, 2015

MAHUDHURIO HAFIFU YAMDUWAZA MKUU TUDARCO



Mkuu wa chuo cha Tumaini Dar es salaam (TUDARCO) profesa Uswege Minga ameshangazwa na idadi kiduchu ya wanafunzi waliohudhuria katika kikao kilichofanyika leo kati yake na wanafunzi.

Akifungua kikao hicho mkuu huyo wa chuo cha TUDARCO ameshangazwa na hali ya wanachuo kutokuhudhuria kikao  hicho kutoka na ukweli kwamba nafasi yake kukut ana na wanachuo kujadili maswala mbalimbali chuoni hapo  kuwa finyu na adimu.



Aidha baadhi ya wanachuo walioshindwa kuhudhuria kikao hicho ambao majina yao pamoja na vitivo vyao havikuweza kufahamika kwa haraka wameonyeshwa kukerwa na kitendo cha serikali ya wanafunzi chuoni hapo (TUSODARCO) kwa kushindwa kupanga siku na muda ambao idadi kubwa ya wanachuo wangeweza kuhudhuria.


Kutokana na ukweli kwamba siku ya ijumaa  katika muda uliopangwa idadi kubwa wanachuo  hawana vipindi na kutokuwepo katika eneo la chuo.

Kikao hicho kimefanyika siku ya leo katika majira ya saa 10 alasiri katika ukumbi wa mikutano uliopo katika chuo hicho.Na kimekuwa cha kwanza kuwakutanisha wanachuo pamoja na uongozi wa chuo cha TUDARCO baada ya kupita mihula(semisters) takribani sita.

No comments:

Post a Comment