Pages

Thursday, July 2, 2015

PROFILE YA JACQUELINE DASTAN



Imeandaliwa na Jay4
  “Mjini mipango” ni moja ya kauli maarufu sana kwa watu watafutaji wa maisha na wenye hasira ya maisha. Ndivyo ilivyo kwa watu wenye kufikiri mbali ya pale walipo na kufikiri zaidi katika maarifa wapatayo yatakuwa na msaada gani katika maisha ya baadae. Mwanamke mchapakazi, muangaikaji na mkombozi kwa wanawake alipata nafasi ya kukutana na mwandishi katika maswali matano.

1.      Unaitwa nani?
“Naitwa Jacqueline Dastan Shinado. Ni mwanafunzi wa mwaka wa pili katika kozi ya BBA (Bachelor of Bussiness Administration). Napatikana Instagram kama (JACQUELINE DASTAN, Fabrajay_10).
Tayari kwenda katika biashara. Picha na Jay4


2.      Unaridhika na huduma ya kiwango cha elimu kinachotolewa na Chuo Kikuu Cha Tumaini?
“Ndio naridhika, kwa kuwa mfumo wa hapo awali ulionikuza kuelewa darasani ndo sawa niliokuta hapa chuoni. Walimu nawaelewa na wamekuwa msaada kwa wanafunzi popote unapowahitaji. Hii imepelekea hata Chuo kuwa na jina kubwa na zuri mtaani na kwenye soko la ajira kwa ujumla”.

3.      Nani ‘Role modal’ wako?
“Oooh!! ‘Role modal’ wangu ni mama yangu mzazi tu, Leah Mbunda.

Mama Leah Mbunda katika pozi. Picha na Jay4


4.      Kwanini Mama yako?
“Nina mengi ya kumuelezea kiukweli, ila kwa upande wa taaluma ni mwanamke ambae yupo tayari kufanya chochote kuhakikisha naenda shule na kupata elimu nzuri. Pia maisha yake aliyoyapitia najiona napita zile njia yeye alizopitia mpaka kuwa hapa. Najivunia sana kuwa mwanae”.






5.      Wewe ni nani baada ya miaka mitano?
“Kwanza mimi ni mfanyabiashara mkubwaa, kuanzia hapa nilipo japo nasoma ila naendesha biashara tofauti  mfano kuuza suruali, vipodozi na mikoba ya wanawake.  Nafanya kwa kusambaza bidhaa kwa kutumia gari langu au natembea nazo mwenyewe katika begi.  Nasomea utawala wa Biashara na miaka mitano mbele kikubwa nitachojivunia ni kuwa nina akili kubwa ya kutotegemea ajira ila inategemea katika KUJIAJIRI kutokana na mfumo wa ajira Tanzania, hivyo nitakuwa nimepata ujuzi mkubwa toka darasani utakaoniwezesha kufikia ndoto zangu za kuwa mfanyabiashara kubwa nchini na nje ya nchi. Ushauri kwa wanawake wenzangu ni kujituma ili tusiwekeze akili na nguvu asilimia kubwa katika kuajiliwa ila tuongeze maarifa katika sekta ya kujiajiri”.

No comments:

Post a Comment