Pages

Wednesday, July 1, 2015

MHESHIMIWA KILENZI ATANGAZA NIA RASMI





Mh. Kilenzi(kushoto) akiwa na Meya wa Manispaa ya Ilala Mh. Silaa
Vijana wengi wametangaza nia ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi mkuu ujao wa mwezi Oktoba 2015, ambapo kutakuwa na uchaguzi wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Wabunge na Madiwani.

Kwa kutambua hilo, Bwana Hermani Kilenzi mwanafunzi wa sheria mwaka wa tatu katika chuo cha Tumaini mwenye historia nzuri ya uongozi hususani wa shule tokea shule ya msingi mpaka chuo kikuu, ametangaza nia rasmi ili aweze kuteuliwa na Chama chake Cha Mapinduzi (C.C.M) apate ridhaa ya kuchaguliwa na wananchi kuwa Diwani wa kata ya Kijitonyama.

“Nimeamua kuchukua hatua hii ili niweze kutatua matatizo ya wananchi wangu wa kata ya kijitonyama hasa katika suala zima la usafi, ambapo nitapanga siku maalumu ya kuungana na wananchi wangu tuwe tunafanya usafi katika maeneo yote muhimu”.   Hata hivyo amesema kuwa yuko tayari kushirikiana na wananchi ili waweze kutatua changamoto za maji, kuziba kwa mitaro, na kuzibua chemba za vyoo.

Pia aliongeza kuwa atahakikisha atawatafuta wadhamini ili waweze kuwasaidia vijana na wamama katika shughuli za ujasiriamali, kwani hayo ni makundi ambayo hayana ajira ya uhakika.






No comments:

Post a Comment