Pages

Thursday, July 9, 2015

MAJI NI UHAI

Maji ni uhai
Ni jambo ambalo kila mtu analijua kutokana na umuhimu wake mkubwa katika maisha ya kila siku ya mwanadamu yeyote ambaye kwa namna moja ama nyingine amejaliwa kuvuta pumzi (ambaye anaishi.)
Maji yanafaida nyingi sana kwa mwanadamu ikiwa ni katika matumizi yake ya kila siku kama vile kunywa na kufanyia shughuli mbali mbali za nyumbani kwa mfano kupika, kuosha vyombo na kufanya usafi wa hapa na pale. Matumizi ya maji hayaishii hapo tu bali yapo mengine hata katika viwanda ambapo maji yanatumika kwa shughuli mbali mbali kutokana na kiwanda husika
Bila kwenda mbali sana, katika mwili wa mwanadamu maji yanachukua nafasi kubwa hii ni pamoja na umuhimu wake katika utendaji kazi wake. Maji katika mwili yanachukua hadi kufikia asilimia takriban 60 ambazo hutumika hasa katika kuupa mwili nguvu kwa kupunguza kiasi cha joto mwili. kazi nyinginezo nyingi za maji ni katika maswala ya kiafya ambapo hutumika kama dawa kwa baadhi ya magonjwa kwa kuzingatia ushauri kutoka kwa wataalamu wa afya waliobobea. Kumbuka hizo ni kazi chache tu za maji na zipo nyingine nyingi.
Amini husiamini, ingawaje maji yanaonekana kuutawala sana uso wa Dunia kwa asilimia takribani 71 lakini yale yanayoweza kutumia na mwanadamu ikiwa na maana ya MAJI SAFI NA SALAMA KWA KUNYWA yanachukua asilimia chache ambazo ni takriban 2.5 tu.
Hivyo basi ni vyema kabla ya kutumia maji kwa kunywa kujua kwamba yanafaa kwa kwa matumizi hayo kwa maana si maji yote uyaonayo baharini, ziwani, mtoni na kwingineko yanapopatikana yanafaa kwa kunywa yakupasa kutambua ni asilimia chache tu yafaayo kwa kunywa.


No comments:

Post a Comment