Pages

Tuesday, August 11, 2015

MAANDALIZI YA SHIMIWI YAPAMBA MOTO



Dar es Salaam.
Shirikisho la Michezo (SHIMIWI) linatarajia kuzindua mashindano ya michezo yatakayoshirikisha watumishi wa Serikali kutoka katika Wizara, Idara zinazojitegemea, wakala wa Serikali na Ofisi za Wakuu wa Mikoa

Akitoa taarifa hiyo kwa waandishi wa habari Katibu Mkuu Kiongozi na Mkuu wa Utumishi wa Umma Balozi Ombeni Sefue alisema mashindano hayo yatafanyika mjini Morogoro kuanzia tarehe 15 hadi 29 Agosti, 2015. Mpaka sasa vilabu  ambavyo vimejitokeza kushiriki mashindano hayo ni 47 tu.

Mashindano hayo yatahusisha vilabu kutoka wizarani ambavyo ni; Ikulu, Utumishi, Waziri Mkuu, Afya, Ardhi na Makazi, Elimu na mafunzo ya Ufundi, Hazina, Kilimo na Chakula. Vilabu vingine ambavyo vitashiriki ni kutoka Wizara ya Mifugo, Wizara ya Maji, Wizara ya Afrika Mashariki, Wizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Mambo ya nje, Wizara ya Mambo ya ndani, Wizara ya Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Wizara ya Viwanda na Biashara, Wizara ya Uchukuzi, Wizara ya Ujenzi, na Tume ya Mipango.

Makuka ameongeza kuwa vilabu vingine ambavyo vitashiriki katika mashindano hayo ni kutoka katika idara mbalkimbali ambavyo ni Idara ya Mahakama, Idara ya Utumishi wa Umma, Ofisi ya Bunge, Tume ya kurekebisha Sheria, Tume ya Mahakama, Ofisi ya Taifa ya Ukaguzi (    NAO), na Tume ya Ushirika.

Vilabu vingine ambavyo vimejiunga kushiriki Mashindano hayo ni vilabu kutoka katika wakala mbalimbali ambavyo ni Wakala wa Jiolojia Tanzania, (GST), Wakala wa Ukaguzi wa Madini (TAA), na Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA),

Pia alisema kutakuwa na vilabu kutoka katika Ofisi za Wakuu wa Mikoa ambavyo ni; Lindi, Katavi, Mwanza, Kagera, Rukwa Dar es Salaam, Mtwara, Iringa, Geita, Kigoma, Manyara, Mara, Arusha na Tanga.

Vilabu ambavyo vitafungua mashindanoi hayo ni Wizara ya Elimu dhidi ya Hadhina (Mpira wa miguu), Wizara ya Afya dhidi ya Wizara ya Mambo ya nfdani(Mpira wa mikono), GTS dhidi ya Wizara ya Mambo ya nje (kuvuta kamba kwa Wanaume), na Ikulu dhidi ya Bunge (kuvuta kamba kwa wanawake. Mashindano hayo yote yataanza muda mmoja ambao ni saa 4:00 Asubuhi.

No comments:

Post a Comment