Pages

Thursday, July 16, 2015

MAGANGA JAPHETI APANIA KUCHUKUA JIMBO LA GEITA MJINI


Bwana Maganga akiwa  anafanya kazi zake kwa umakini  kuubwa

    Idadi wa Wanafunzi wa Chuo kikuu cha Tumaini wanaowania nafasi mbalimbali za uongozi wa ubunge na udiwani zinazidi kuongezeka kadri ya siku zinavyozidi kwenda.

   Mmoja wa wanaowania nafasi hizo ni Bwana Maganga Japheti Emmanuel ambaye ni mwanafunzi wa Ualimu mwaka wa tatu, ametia nia rasmi ya kutaka kugombea ubunge katika jimbo la Geita  mjini kupitia chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA).

   Akiongea na mwandishi wa mainkampasi.blogspot alisema, “Nina kila sababu ya kutaka kugombea ubunge katika jimbo la Geita ili niweze kuwaokoa wananchi wangu ambao ni maskini wakati wana rasilimali za kutosha hasa mgodi wa madini wa Geita (Geita Gold Mine), pamoja na uwepo  wa hifadhi ya Taifa ya Rubondo ambazo huingiza mapato makubwa.” 

   Hata hivyo alisema kuwa, mtu anayetaka kugombea katika jimbo la Geita lazima azijue shida za watu wa Geita na namna ya kuzitatua, lakini wabunge wote waliopita wameshindwa kuzitatua ili hali kuna rasilimali za kutosha badala yake hujinufaisha wao wenyewe.

   Bwana Maganga ameongeza kuwa  CHADEMA ambayo ipo ndani (UKAWA),  ndiyo chama pekee ambacho kinajua matatizo ya wananchi na namna ya kuyatatua, na wananchi wameteseka kwa miaka mingi kupitia Chama Cha Mapinduzi  (CCM), hivyo huu ni mwaka wa ushindi na mafanikio kwa wananchi  kupitia CHADEMA.  

   Pamoja na hayo yote amesema kuwa amekuwa ndani ya chama kwa miaka mingi na anajua mengi kuhusu chama chini ya uongozi  shupavu wa Mwenyekiti Freeman Mbowe, ambaye  ameweza kutatua matatizo mengi na kuleta mafanikio makubwa katika chama.



No comments:

Post a Comment