Pages

Wednesday, July 22, 2015

KARIBUNI CHUO KIKUU TUMAINI



Wanafunzi wapya wanaojiunga na kozi mbalimbali katika Ngazi ya cheti na Diploma katika Chuo Kikuu cha Tumaini Dar es salaam, wameaswa kutumia muda wao vyema katika kipindi cha masomo yao.
Dr, Loth akizungumza na baadhi ya wanafunzi

Akizungumza na wanafunzi hao wakati wa hafla ya kuwakaribisha Dr Gillard Loth ambae ni Muhadhili wa Chuo kikuu cha tumaini katika masomo ya Uchumi na Rasilimali watu, ametaja baadhi ya mambo ambayo yana changia kupoteza muda kwa wanafunzi kama vile simu za mikononi, urafiki uliopitiliza na Foleni.
Baadhi ya wanfunzi wakiwa katika hafla ya kukaribishwa

Pia akinukuu Maneno matakatifu kutokwa kwenye Biblia Eph3:20 Loth amesema Mungu ameweka mambo Mengi sana ndani yamwanadamu na hivyo kuna ulazima wa kumtegemea Mungu katika masomo na maisha ili kufikia malengo walio yaweka
Loth amesisitiza kuwa muda wa kuwapo chuoni ni mchache sana na hivyo ni vyema kutumia muda huo waliopata katika kujisomea ilikutimiza malengo yao. Pia amesisitiza katika nidhamu baina ya wanafunzi na wanafunzi pia kwa wafanya kaziwa Chuo.
Katika kuhakikisha kuwa wanafunzi wapya wanajua wanayotakiwa kufanya Loth amewakumbusha kusoma kwa bidii wawapo darasani, kujisomea vitabu ili kupanua uwezo wa kufikiri akitolea mfano wa vitabu vya Think Big na Gifted Hands cha mwandishi Ben carson na zaidi wametakiwa kuhudhuria vipindi vya darasani.
Dean of Students Mama Lema
 Pia moja ya mwanafunzi Francis Sylvester amesema amechagua kujiunga na Chuo cha Tumaini sababu ya Nidhamu inayopatikana Chuoni hapo na pia Elimu bora ambapo ametolea mfano wa kaka yake kuwa ni mmoja ya Tunda la Chuo kikuu cha tumaini Dar es salaam na anafanya vizuri katika soko la Ajira kama Mwanasheria.
Francis Sylvester
MAINKAMPASI tunawatakia kila lakheri katika masomo yenu, penye nia pana njia!

5 comments:

  1. TUNAWAKALIBISHA SANA CHUONI KWETU,,,,,,MAHITAJI MUHIM YANAYOTAKIWA KWA WANFUNZI YANAPATIKANA HAPA,,,,,

    ReplyDelete
  2. TUNAWAKALIBISHA SANA CHUONI KWETU,,,,,,MAHITAJI MUHIM YANAYOTAKIWA KWA WANFUNZI YANAPATIKANA HAPA,,,,,

    ReplyDelete
  3. karibuni sana wapendwa all are possible

    ReplyDelete