Pages

Monday, July 20, 2015

JIMBO LA PERAMIHO LIMEPATA MUOKOZI



 Solanus Elenziary Gumbo
 Solanus Elenziary Gumbo, ambaye ni mhadhiri wa chuo Kikuu cha Tumaini cha Dar es Salaam ametangaza nia rasmi ya kugombania ubunge kupitia chama cha demokkrasia na maendeleo (CHADEMA) katika jimbo la Peramiho mkoani Ruvuma.

Akizungumza na mainikampasi amesema kuwa,  ndani ya miaka miwili ya mwanzo atakuwa ametimiza takribani asilimia 50 ya sera zake. Elimu yake ya Sekondari ameipata Seminari,  mara baada ya kuhitimu kidato cha sita alijiunga na Seminari kuu kwa ajili ya elimu ya filosofia na theologia, baadae akasoma shahada ya ualimu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, na amesomea shahada ya udhamivu ya taaluma ya maendeleo  katika chuo hichohicho.

Amejiunga na CHADEMA mwaka 2007, “Kilichonipelekea kujiunga na CHADEMA ni kutokana na sera nzuri za chama na ziko kivitendo zaidi, kulinganisha na vyama vingine, pia kuwepo kwa viongozi shupavu ndani ya chama kama vile  Halima Mdee, Tundu Lissu, Dr. Wilbroad  Slaa na wengineo wengi” aliongeza bwana Gumbo.

Amesema kuwa, atahakikisha anasimamia suala la elimu kwa shule zote za msingi na Sekondari, pia walimu wanapata nyumba nzuri na za kudumu pamoja na upatikanaji wa vitabu vya kwa ajili ya shule zote katika jimbo la Peramiho pamoja na, walimu wa kutosha na upatikanaji wa maabara  na mabweni katika shule zote  za Sekondari ili kuinua kiwango cha ufaulu katika jimbo lake.
Gumbo akionesha ishara ya amani na upendo

 Pia ameahidi kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo ili waweze kuwasaidia wananchi katika shughuli za ujasiriamali na, atahakikisha wananchi wa Jimbo lake wanapata umeme, kwani wamehangaika kwa muda mrefu wakisubiri umeme tangu enzi za uhuru (1961) mpaka sasa hawajaletewa,“hatuwezi kuwa na maendeleo bila ya uwepo wa umeme ona nchi zote zilizoendelea kama Ujerumani, Chiina na Ufaransa ni kutokana na uwepo wa umeme na hii inawezekana ndani ya nchi yetu”, alihoji

No comments:

Post a Comment