
Ripoti zinasema kuwa Mourinho, 52 alikua tayari kusaini mkataba mpya baada ya kufurahia msimu uliopita kwa kutwaa ubingwa wa England na Kikombe cha Ligi akiwa na kikosi hicho. Mourinho alirudi Chelsea baada ya kuzifundisha kwa mafanikio klabu za Inter Milan ya Italia na Real Madrid ya Hispania.
Chelsea itaanza kampeni ya kutetea ubingwa wake kesho itakapoivaa Swansea City katika dimba la Stamford Bridge.
No comments:
Post a Comment